Skip to main content

Gavana Joho na hasimu wake wa kisiasa Suleiman Shahbal wazika tofauti zao za kisiasa



Gavana wa Mombasa Ali Hassan Joho akisalimiana na hasimu wake wa kisiasa Suleiman Shahbal. PICHA Mwarandu Randu
Mwarandu Randu na Godfrey Aluda

Gavana wa kaunti ya Mombasa Ali Hassan Joho na hasimu wake wa kisiasa Suleiman Shahbal wameamua kuzika tofauti zao za kisiasa kwa manufaa ya wakaazi wa kaunti ya Mombasa.

Wakizungumza na wanahabari leo katika afisi za gavana hapa jijini  Mombasa, Joho amesema kuwa tofauti za kisiasa sio kigezo cha kutengana na kuwekeana uadui baina yao.

Joho amedokeza kuwa ataendelea kufanya majadiliano ya mara kwa mara na mpinzani wake ili kutafuta suluhu  la  kudumu kwa changamoto zinazowakabili wakaazi wa Mombasa.

Hata hivyo gavana huyo amepongeza mwafaka wa maelewano baina ya rais Uhuru Kenyatta na kinara wa upinzani Raila Odinga.

Wakati uo huo, Suleiman Shahbal amewataka viongozi wa ukanda wa pwani kuzika tofauti zao za kisiasa na badala yake waangazie miradi ya maendeleo.

Shahbal hata hivyo ameitaka serikali kuu kuwapa kipaumbele wawekezaji wa humu nchini wakati wa kutekelezwa kwa mradi wa Dongo Kundu.

Amesema kuna haja ya serikali kuu kuzingatia kikamilifu wawekezaji wa humu nchini huku akisistiza kuwa wana uwezo wa kuteleleza mradi huo.

Gavana Joho Suleiman Shahbal na Gavana wa Nairobi Mike Sonko
Kwa upande wake gavana wa kaunti ya Nairobi Mike Mbuvi amewahimiza viongozi nchini kukumbatia mwafaka huo ili kuwanunganisha wananchi mashinani.

Aidha Sonko amewapongeza viongozi hao kwa kukubali kuweka kando tofauti zao za kisiasa na kuamua kushirikiana katika kukuza uchumi wa kaunti ya Mombasa.

Itakumbukwa kwamba gavana joho na Suleiman Shahbal walikuwa mahasimu wa kisiasa katika uchaguzi mkuu uliopita.




Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Involve all stakeholders when proposing new laws- BOTTAX General Secretary petitions government

BOTTAX General Secretary Cynthia Wanyonyi Photo (courtesy) BY PETER KOMBE Kenya Boda Boda Tuk Tuk and Taxi Workers Union (BOTTAX Kenya) has faulted the government on claims of passing bills that do not favor the transport sector. Speaking to the media in Mombasa on Monday the union’s General Secretary Cynthia Wanyonyi said in most cases the government does not involve boda boda Tuk Tuk and other informal transport worker's representatives. She further noted that as stakeholders in the public transport sector the government fails to carry out effective public participation exercises as enshrined in the Kenyan constitution. “The government does not involve the public when making certain decisions,” she noted. Wanyonyi urged both the operators to register with the union to avoid being misled by what she claims are quack organisations. She urged the department concerned with registering cooperatives and other associations touching on the informal trans...

MALONZA AIDHINISHWA

Sasa ni afueni kwa waziri mteule wa utalii Peninah Malonza baada ya bunge la kitaifa kuidhinisha majina yote ya mawaziri wateule ikiwemo la Bi. Malonza. Malonza alinusuriwa baada ya bunge kukataa pendekezo la kamati hiyo kuwa asiidhinishwe. Wabunge wa mrengo wa Kenya Kwanza, waliunga mkono kuidhinishwa kwa Malonza, wakisema ana tajiriba ya kutosha na anapaswa kupewa fursa ya kuhudumu. Sasa majina ya mawaziri wateule walioidhinishwa yatawasilishwa kwa rais kwa uteuzi rasmi.

Mombasa county government commits ksh 3.5 million on FP in 2018-2019 financial year- says County adolescent coordinator

County AYSR coordinator Baraka Imani facilitating the session at Pride Inn Mombasa on Tuesday Photo by Peter Kombe   BY PETER KOMBE The county government of Mombasa has committed a financial kitty of ksh 3.5 million to boost family planning in the 2018 2019 financial year. The funds according to the county adolescent coordinator Baraka Imani will addressing some of the challenges that Mombasa locals face on issues of family planning. “The county government has committed a total of 3.5 million to boost FP uptake in Mombasa county” Baraka Imani county adolescent coordinator said Out of the 3.5 million the county has committed, a total of ksh 500,000 targets Adolescents’ Young and Sexual Reproductive Health (AYSRH) Speaking to the media in Mombasa on Tuesday Mombasa County adolescent and youth sexual reproductive officer Baraka Imani said the county is currently implementing two programs including family planning and AYSRH. “A total of ksh 500,000 has tar...