Skip to main content

Shirika la Haki Afrika laishinikiza serikali ya Kenya na Tanzania kutafuta suluhu la haraka kufuatia kuzuiliwa kwa Hamisi Zuma.

Afisa wa kitengo cha dharura kutoka shirika la Haki Afrika Mathias Shipeta Picha (Maktaba)
Na Mwarandu Kombe

Shirika la kutetea haki za binadamu la Haki Afrika limeitaka serikali ya Kenya na Tanzania kuingilia kati ili kutafuta suluhu la haraka kufuatia kuzuiliwa kwa mkenya Hamisi Zuma Madilo nchini Tanzania.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari afisa wa kitengo cha dharura wa shirika hilo Mathius Shipeta amesema shirika hilo limeghadhabishwa na hatua ya serikali ya Tanzania kumzuilia mkenya huyo asiyekuwa na hatia.

Ameongeza kuwa licha ya mataifa ya Kenya na Tanzania kutia saini mkataba wa wa makubaliano  baina ya nchi hizi mbili maeneo ya mpakani  bado mkataba huo unakiukwa.

Ametaja hatua ya kumzuilia mkenya huyo kama ukiukaji mkuu wa haki za binadamu.

Kulingana na taarifa ya hivi punde kutoka kwa afisa huyo maafisa wa shirika hilo wakiandamana na familia ya mhusika wako eneo la Horo Horo nchini Tanzania.

Mkenya huyo alikamatwa na maafisa wa mpakani nchini Tanzania usiku wa kuamkia siku kuu ya krismasi huku akiendelea kuzuiliwa hadi sasa.

Amezitaka idara husika nchini Tanzania kuheshimu sheria na haki za kibinadamu na kumuachilia huru mkenya huyo.


Comments

Popular posts from this blog

Involve all stakeholders when proposing new laws- BOTTAX General Secretary petitions government

BOTTAX General Secretary Cynthia Wanyonyi Photo (courtesy) BY PETER KOMBE Kenya Boda Boda Tuk Tuk and Taxi Workers Union (BOTTAX Kenya) has faulted the government on claims of passing bills that do not favor the transport sector. Speaking to the media in Mombasa on Monday the union’s General Secretary Cynthia Wanyonyi said in most cases the government does not involve boda boda Tuk Tuk and other informal transport worker's representatives. She further noted that as stakeholders in the public transport sector the government fails to carry out effective public participation exercises as enshrined in the Kenyan constitution. “The government does not involve the public when making certain decisions,” she noted. Wanyonyi urged both the operators to register with the union to avoid being misled by what she claims are quack organisations. She urged the department concerned with registering cooperatives and other associations touching on the informal trans...

MALONZA AIDHINISHWA

Sasa ni afueni kwa waziri mteule wa utalii Peninah Malonza baada ya bunge la kitaifa kuidhinisha majina yote ya mawaziri wateule ikiwemo la Bi. Malonza. Malonza alinusuriwa baada ya bunge kukataa pendekezo la kamati hiyo kuwa asiidhinishwe. Wabunge wa mrengo wa Kenya Kwanza, waliunga mkono kuidhinishwa kwa Malonza, wakisema ana tajiriba ya kutosha na anapaswa kupewa fursa ya kuhudumu. Sasa majina ya mawaziri wateule walioidhinishwa yatawasilishwa kwa rais kwa uteuzi rasmi.

Mombasa county government commits ksh 3.5 million on FP in 2018-2019 financial year- says County adolescent coordinator

County AYSR coordinator Baraka Imani facilitating the session at Pride Inn Mombasa on Tuesday Photo by Peter Kombe   BY PETER KOMBE The county government of Mombasa has committed a financial kitty of ksh 3.5 million to boost family planning in the 2018 2019 financial year. The funds according to the county adolescent coordinator Baraka Imani will addressing some of the challenges that Mombasa locals face on issues of family planning. “The county government has committed a total of 3.5 million to boost FP uptake in Mombasa county” Baraka Imani county adolescent coordinator said Out of the 3.5 million the county has committed, a total of ksh 500,000 targets Adolescents’ Young and Sexual Reproductive Health (AYSRH) Speaking to the media in Mombasa on Tuesday Mombasa County adolescent and youth sexual reproductive officer Baraka Imani said the county is currently implementing two programs including family planning and AYSRH. “A total of ksh 500,000 has tar...