Skip to main content

Gavana Samboja awashtumu wanasiasa kwa madai ya kuwagawanya wakenya kwa misingi ya kikabila




Na Godfrey Aluda / Mwarandu Kombe

Gavana wa kaunti ya Taita Taveta Granton Samboja picha (Maktaba)
Gavana wa Taita Taveta Granton Samboja amewataka viongozi wa kisiasa nchini kutowagawanya wakenya kwa misingi ya kikabila.

Akizungumza leo hapa jijini Mombasa wakati wa ufunguzi rasmi wa kongamano la viongozi wa kaunti hiyo gavana huyo amesisitiza haja ya wanasiasa  kuzingatia maendeleo yatakayowafaa wakenya.

Amesema msimu wa siasa umepita na kilichobaki ni kuwafanyia kazi wakenya.

Wakati uo huo, Samboja ameunga mkono kuchaguliwa kwa gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya kama mwenyekiti wa baraza la magavana nchini.

Samboja aidha amedokeza kuwa kuchaguliwa kwa gavana huyo kulitekelezwa katika njia ya uwazi huru na haki.

Itakumbukwa kuwa hivi majuzi gavana wa kaunti ya Kwale Salim Mvurya alipinga uchaguzi huo akisema kuwa kulikuwepo mkataba wa maelewano ili kumrithi aliyekuwa mwenyekiti wa baraza hilo Josphat Nanok.

Vile vile gavana huyo amesema baraza la magavana litahusika kikamilifu katika mchakato wa kuifanyia marekebisho katiba ili kugatua fedha zaidi mashinani.


Comments

Popular posts from this blog

Involve all stakeholders when proposing new laws- BOTTAX General Secretary petitions government

BOTTAX General Secretary Cynthia Wanyonyi Photo (courtesy) BY PETER KOMBE Kenya Boda Boda Tuk Tuk and Taxi Workers Union (BOTTAX Kenya) has faulted the government on claims of passing bills that do not favor the transport sector. Speaking to the media in Mombasa on Monday the union’s General Secretary Cynthia Wanyonyi said in most cases the government does not involve boda boda Tuk Tuk and other informal transport worker's representatives. She further noted that as stakeholders in the public transport sector the government fails to carry out effective public participation exercises as enshrined in the Kenyan constitution. “The government does not involve the public when making certain decisions,” she noted. Wanyonyi urged both the operators to register with the union to avoid being misled by what she claims are quack organisations. She urged the department concerned with registering cooperatives and other associations touching on the informal trans...

MALONZA AIDHINISHWA

Sasa ni afueni kwa waziri mteule wa utalii Peninah Malonza baada ya bunge la kitaifa kuidhinisha majina yote ya mawaziri wateule ikiwemo la Bi. Malonza. Malonza alinusuriwa baada ya bunge kukataa pendekezo la kamati hiyo kuwa asiidhinishwe. Wabunge wa mrengo wa Kenya Kwanza, waliunga mkono kuidhinishwa kwa Malonza, wakisema ana tajiriba ya kutosha na anapaswa kupewa fursa ya kuhudumu. Sasa majina ya mawaziri wateule walioidhinishwa yatawasilishwa kwa rais kwa uteuzi rasmi.

Learn instrumentals and write your own songs- Eric Wainaina tells upcoming artistes.

Eric Wainaina delivering a keynote address at Aga Khan Academy Mombasa on Saturday during the academy's 13th graduation ceremony   BY PETER KOMBE Eric Wainaina famed for his “Nchi ya Kitu Kidogo” song has told upcoming artistes to learn musical instruments besides writing their own songs. According to him this is the only way to stay relevant in the industry which he terms as being competitive. He says his new album ‘Dreams in Stereo’ is currently available in all digital platforms including mdundo.com, skiza and amazon tunes. The famed artiste says “the new album is one of my fine works.” The artist however denied claims that he was working behind the curtain rather he says he had earlier on produced two albums which according to him did not get good airplay. “The music industry like any other industry has both ups and downs,” he said. The new album “ Dreams in Stereo” is a vivid description of my life, love, passion and betrayal.” Asked wh...